MONDAY, AUGUST 3, 2026

Good morning, reader.

Latest stories from across MsomiHuru

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhandisi Hamad Masauni amesema, Muungano na kati ya vitu ambavyo havipaswi kuchezewa inatakiwa kulindwa kwa hali ya juu.

MWAKA 1992, Tanzania ilirejesha mfumo wa vyama vingi vya siasa tangu kufutwa mwaka 1964. Hatua hiyo ilitarajiwa kuongeza ushindani wa kisiasa, kuimarisha demokrasia na kuwapa wananchi chaguo mbadala la uongozi.

Miaka mitano ya utawala wa Rais Samia Suluhu Hassan imeufungua Mkoa wa Kigoma kwa kufanya ufikike kirahisi, kupunguza gharama za safari na kufungua fursa za kiuchumi kwa wakazi wake.

KABLA ya kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi, jina lake halikuwa kubwa katika siasa za Tanzania. Umaarufu wake ulijengwa zaidi katika kipindi cha mabadiliko hayo ya kisiasa kwenye miaka ya 1990, kwa kuibua hoja mbalimbali ikiwamo ya kutaka mgombea binafsi.

Marekani imetangaza kutosalimu amri kwa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), huku Waziri wa Mambo ya Nje, Marco Rubio akisema taasisi hiyo haina mamlaka kuhusu wananchi wala mfumo wa sheria wa nchi hiyo.

MKOA wa Manyara unatarajia kukusanya Sh. bil. 1.5 katika mbio za hisani Manyara Tanzanite Marathon, ili kusaidia kununua vifaatiba na kujenga jengo la watoto njiti kuokoa maisha yao.

Wananchi wa Zanzibar watalazimika kujiandaa na gharama mpya za usafiri wa daladala kuanzia Agosti mosi, 2026, baada ya serikali kutangaza ongezeko la nauli katika ruti mbalimbali za Unguja na Pemba.

Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, amemtaka mkandarasi anayejenga barabara mkoani Morogoro kufuata masharti ya mkataba la sivyo utavunjwa na kampuni hiyo kupigwa marufuku kupewa kazi yoyote nchini.

CHAMA kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Wilaya ya Tunduru (TAMCU), kimesema kuwa hadi mnada wa nane na wa mwisho kwa msimu wa mwaka 2026/2027 kimeuza kilo 2,147,796 zenye Sh. bilioni 5.3

ZAIDI ya wananchi 240 kati ya watu 510 waliopimwa afya zao katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF), maarufu Sabasaba, yaliyodumu kwa takribani wiki mbili, waligundulika kuwa na shinikizo la damu (presha) au kisukari bila kufahamu hali zao za kiafya.

WASICHANA 50 wamejiunga na programu ya kinara ya maendeleo ya biashara (enterprise development),ili kuwezesha kizazi cha vijana kinachounda utajiri, kwa kuwapatia ujuzi kwa vitendo, kuendesha biashara zenye ushindani na kubaini fursa za masoko.

Shahidi wa tisa katika kesi ya uchaguzi inayomkabili mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini Clayton Chipando (BabaLevo) Rehema Said amekana maelezo katika ukurasa wa 11 wa hati yake ya ushahidi akidai kuwa si ya kwake.

Markets, companies and money stories

Business stories will appear here once published.

Sports news and analysis

Sports stories will appear here once published.

Hand-selected by our newsroom

Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amewahimiza wafanyabiashara nchini kutumia maonesho ya Kimataifa ya Sabasaba kama jukwaa la kutangaza bidhaa na huduma zao kwa kujenga ushirikiano wa kibiashara na kuvutia wawekezaji kutoka nje ya nchi.

CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ni chuo kikuu cha umma na kongwe na kikubwa zaidi nchini.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila amewahamasisha wananchi kuendelea kutembelea Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), akisema maonesho hayo yameendelea kuvutia idadi kubwa ya watu wanaokwenda kujifunza, kununua bidhaa na kupata huduma mbalimbali za kijamii.

Watu wanne wamefariki dunia na wengine 14 wakijeruhiwa katika ajli ya barabarani iliyotokea leo Julai 7, 2026 majira ya asubuhi katika Kata ya Chem Chem mkoani Tabora ikuhusisha basi la abiria lenye namba za usajili T384 DGF mali ya kampuni ya Last Bullet lililokuwa likitoka Mkoani Tabora kuelekea Mkoani Geita.

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Dk. Rhimo Nyansaho, amesema Shirika la Uzalishaji Mali la JKT (SUMAJKT), linaendelea kutoa mchango kwa nchi, hasa kupunguza tatizo la ajira kwa vijana kupitia kampuni zake tanzu.

Kutokana na uwepo wa tishio la maandamano leo Julai 7, baadhi ya shughuli za kiuchumi za kila siku zimedorora kutokana na wananchi kuwa na hofu huku wengine wakishindwa kwenda kwenye majukumu yao huku wafanyabiashara na wajasiriamali wakishindwa kufungua maduka.

Zanzibar inatarajiwa kuandika ukurasa mpya katika historia ya siasa zake baada ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, kutarajiwa kushuhudia hafla ya uwasilishaji wa Tamko la Pamoja la Maridhiano ya Kisiasa kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ACT-Wazalendo.

Mwanafunzi aliyetekwa apiga simu

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umeendelea kuimarisha juhudi za kupanua wigo wa hifadhi ya jamii nchini kwa kuwahamasisha wananchi waliojiajiri kujiunga na Hifadhi Skimu, huku ikiwahimiza waajiri wenye malimbikizo ya michango kunufaika na msamaha wa tozo uliotolewa na mfuko huo.

TANZANIA na Angola, zimesema kuna haja ya kuugeuza uhusiano mzuri wa miaka mingi walionao kuuweka katika matendo katika kushirikiana kwenye biashara na uwekezaji, ili kuzalisha ajira nakuchochea ukuaji wa uchumi kwa nchi hizo mbili.

MRISHO Hassani Nagwenya (13), mkazi wa Mtaa wa Boma, Kata ya Magengeni, Tarafa ya Mikindani, Manispaa ya Mtwara-Mikindani, amefariki dunia, baada ya kuzama baharini.

WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba, amemwagiza Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi, kuwafuatilia na kuwabaini watu wanaoendeleza mijadala kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka 2030 badala ya kujikita katika shughuli za maendeleo.